Zitto Ataka Hatua Kali Zichukuliwe Dhidi ya Askari Polisi Aliyemtishia Bunduki Adam Malima

Aliyekuwa Naibu Waziri Wizara ya Fedha katika utawala wa awamu ya nne, Adam Malima.
Zitto kabwe ameonyesha masikitiko hayo kupitia ukurasa wake wa kijamii Facebook akihoji kama polisi wanafundishwa kuwafanyia hivyo raia wasiokuwa na hatia kiasi cha kuibua hofu katika jamii inayowazunguka na kupoteza imani na jeshi hilo la polisi.
“Hii ni nini ?, askari wetu wanafundishwa kufanya hivi, Waziri Mwigulu huyu yupo wazi na ni wa kutoka kwako. Unahitaji uchunguzi”. Ameandika Zitto.
Zitto aliandika hayo baada ya muda mchache kupita kwa tukio hilo 
lililowahusisha askari hao walioambatana na kampuni ya Majembe Auction 
Mart waliokuwa wakitaka kujaribu kukamata gari iliyokuwa imeegeshwa 
pembeni ya barabara ya Masaki karibu na Hoteli ya Double tree ingawa 
ndani ya gari hilo alikuwepo dereva.
 

No comments