Said Mecki Sadiki Ataja Sababu Zilizomfanya Aandike Barua Ya Kuacha Kazi ya Ukuu wa Mkoa

Aliyekuwa Muu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Mecki Sadiki , amesema ameamua kuondoka serikalini baada ya utumishi wa muda mrefu na anakwenda kupumzika mkoani Mwanza huku akiwa mfugaji wa samaki.
Aidha
 Sadiki alisema pia kulingana na afya yake, anahitaji kupisha vijana 
wadogo wamsaidie Rais Dk John Pombe Magufuli kulingana na kasi yake 
kwani yeye ameepuka kumkwaza rais wakati wa utekelezaji wa majukumu yake
 kama mkuu wa mkoa. 
“Uamuzi
 huu wa kupumzika nilimuomba rais kwa muda mrefu sana, na nikirudi 
kijijini nitaendelea na ufugaji Samaki maana nilishaandaa bwawa la 
kufugia, nitaendelea nalo huku nikiwaza jambo lingine la kufanya,” alisema.
Sadiki
 alisema hayo jana wakati akitaja sababu zilizochangia kumuomba Rais 
Magufuli kuacha kazi yake ya ukuu wa mkoa wa Kilimanjaro. 
“Namshukuru
 rais kuridhia ombi langu, nimetumikia serikali tangu mwaka 1999 nikiwa 
mkuu wa wilaya na baadaye mkuu wa mkoa kuanzia mwaka 2005 hadi sasa 
ninapoondoka mwenyewe... nimeona ni wakati muafaka kumweleza aliyeniteua
 kuwa nahitaji kupumzika nikiwa na akili timamu na afya njema,” alisema.
Alisema
 Sababu nyingine kubwa ni kuhofia afya yake kutomudu kasi ya rais 
Magufuli, kwani alifanywa upasuaji mwaka 2012 na 2014 nchini India 
ingawa hakutaka kuweka wazi maradhi yaliyokuwa yakimkabili. 
“Kama
 kiongozi muungwana lazma ifike mahali ukiri kwamba wapo vijana wenye 
uwezo mzuri na kasi ambayo inaendana na serikali ya awamu ya tano... 
mimi nilishatekeleza wajibu wangu na mchango kwa serikali yangu, sasa 
inatosha, tupate mawazo na michango ya wengine,” alisema.
Sadiki
 ambaye amekuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro tangu Machi 13,2016 
alipoteuliwa na Rais Magufuli, alisema siyo vibaya kwa kiongozi 
kujitathmini na kuwaachia wengine kama atabaini kasi yake ya utendaji 
kazi imeanza kupungua. 
Kwa
 mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, 
Ikulu, Gerson Msigwa, mkuu wa mkoa Sadiki pamoja na aliyekuwa jaji wa 
Mahakama Kuu ya Tanzania na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebeisha Sheria 
Tanzania, Aloysius Mujulizi na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Upendo 
Msuya waliomba kuacha kazi na rais akaridhia
No comments