TANZANIA YAKUBALI KUPELEKA WALIMU WA SOMO LA KISWAHILI RWANDA
Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli amepokea barua yenye ujumbe wa Rais 
wa Jamhuri wa Rwanda Mhe. Paul Kagame iliyowasilishwa kwake na Mjumbe 
Maalum ambaye ni Waziri wa Elimu wa Rwanda Dkt. Musafiri Papias Malimba.
Pamoja na kupokea barua hiyo, Mhe. Rais Magufuli na Dkt. Musafiri Papias
 Malimba wamezungumzia masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya 
Tanzania na Rwanda ikiwemo katika sekta ya elimu hususani maendeleo ya 
sayansi na teknolojia.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameipongeza Rwanda kwa kuamua lugha ya 
Kiswahili ianze kufundishwa katika shule zake na ameahidi kuwa Tanzania 
ipo tayari kutoa walimu wa kwenda kufundisha lugha hiyo.

No comments