Manusura wa Lucky Vicent aliyefanyiwa upasuaji wa uti wa mgongo aonyesha dalili njema.
Manusura
 wa ajali ya Lucky Vincent, Doreen Mshana, amepata hisia katika miguu 
yake yote miwili, ikiwa ni siku chache tangu afanyiwe upasuaji mkubwa wa
 uti wa mgongo.Hiyo ni ishara kuwa upasuaji mkubwa wa uti wa mgongo 
aliofanyiwa, umefanikiwa.
Wenzake
 Wilson Tarimo na Saidia Ismael wameruhusiwa baada ya kupata matibabu na
 sasa wanaendelea na mazoezi ya viungo katika nyumba maalum kwa wagonjwa
 waliovunjika viungo jijini Sioux.Walikuwa wamelazwa katika Hospital ya 
Mercy Sioux City, Marekani walikokuwa wakipata matibabu baada ya ajali 
mbaya ya basi iliyoua wanafunzi wenzao 32, Mei 6 mwaka huu.
Mbunge
 wa Singida Kaskazini(CCM) Lazaro Nyalandu, amesema Doreen ameweza 
kuisogeza miguu yake miwili kwa mara ya kwanza tangu apate ajali 
hiyo.“Tuendelee kumuombea,huu ni uponyaji wa uti wake wa mgongo.” 
amesema Nyalandu katika mtandao wake wa facebook.Pia watoto Saidia na 
Wilson, pamoja na wazazi wao, walikwenda Hospitali kumuangalia Doreen 
leo  ambaye bado amelazwa akiendelea na matibabu.
No comments