KESI YA WEMA SEPETU KUTUMIA BANGI YAPIGWA KALENDA
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini 
Dar es Salaam, imeambiwa kwamba upelelezi wa kesi ya kukutwa na bangi 
inayomkabili Muigizaji maarufu, Wema Sepetu na wenzake umekamilika.
Hatua hiyo imefikiwa   ambapo upande wa 
Jamhuri mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba alisema kwamba 
upelelezi umekamilika dhidi ya msanii huyo na wakili wa Serikali Helleni
 Mushi aliomba kesi hiyo kuarishwa  na kupangwa tarehe ya kuanza 
kusikilizwa ili watuhumiwa waanze kusomewa maelezo ya awali.
Katika kesi ya msingi, Wema anatuhumiwa 
kukutwa na msokoto mmoja wa bangi na vipande viwili vidogo vya bangi 
vyenye uzito wa gramu 1.08. 
Mbali na Wema washitakiwa wengine ni 
wafanyakazi wake wa ndani Angelina Msigwa (21) na Matrida Abas (16), 
ambapo wote wanashtakiwa kwa kosa moja la kukutwa na kiasi hicho cha 
dawa za kulevya.
Inadaiwa kuwa Wema na wenzake walitenda 
kosa hilo Februari 4 mwaka huu, nyumbani kwao Kunduchi Ununio , Wilaya 
ya Kinondoni Mkoa wa Dar es Salaam.
Hakimu Simba alisema  kesi hiyo itaanza kusikilizwa, Juni Mosi, mwaka kwa watuhumiwa kuanza kusomewa maelezo ya awali.
No comments