Marekani yaituhumu Syria kwa kuchoma wafungwa gerezani

Marekani imeituhumu
 serikali ya Syria kwa kujenga sehemu ya kuchoma maiti katika jela ya 
kijeshi iliyopo karibu na Damascus ili kuficha mauaji ya halaiki ya 
wanaoshikiliwa na serikali.
Wizara ya mambo ya nje ya Marekani 
imeonyesha picha zilizopigwa kupitia njia ya Satelite ambazo imesema ni 
sehemu ya kuchoma maiti katika gereza lililopo Sednaya ambapo Umoja wa 
Mataifa na mashirika ya kutetea haki za binadamu yamesema maelfu ya 
wafungwa wameteshwa na kunyongwa. 
Ameongeza kusema kuwa, mauaji hayo yanafanyika kutokana Syria kuungwa mkono na Urusi na Iran.
Source: BBC Swahili
No comments