Obama atuhumiwa kudukua simu ya rais Trump
Rais
 wa Marekani, Donald Trump amesema kuwa amegundua Rais mstaafu wa nchi 
hiyo ambaye ni mtangulizi wake, Barack Obama alikuwa akidukua simu yake 
mwezi mmoja kabla ya kuchaguliwa kuliongoza taifa hilo.
Rais Trump ametoa shutuma hizo kupitia ujumbe wake wa Twitter Jumamosi ambapo ameandika kuwa: ‘Makosa
 sana! Nimegundua kwamba rais Obama alikuwa akidukua simu yangu katika 
ofisi yangu iliyopo Trump Tower kabla ya mimi kupata ushindi.’
Pamoja
 na shutuma hizo, Rais Trump hajatoa ushahidi wowote ili kuthibitisha 
madai hayo ama hata kusema ni agizo gani la mahakama alilonukuu.
Aidha,
 vyombo vya habari Marekani vimetoa ripoti zinazoeleza kuwa shirika la 
kijasusi la FBI liliomba agizo la kuwachunguza maafisa wa karibu wa Rais
 Trump kutoka kwa shirika la kigeni la kijasusi Fisa kubaini iwapo 
wamekuwa wakiwasiliana na maafisa wa Urusi.
Pamoja na kwamba agizo hilo lilikataliwa lakini baadaye likakubaliwa mwezi Oktoba kulingana na ripoti hizo za vyombo vya habari.


No comments