PICHA: Tembo Waliovamia Chuo Kikuu cha UDOM Waondolewa
Tembo wakiwa wamejificha kwenye vichaka ndani ya eneo la Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) jana. 
Kwa
 mujibu wa taarifa za Wahifadhi wa Wanyamapori inaelezwa kuwa sehemu ya 
eneo hilo litakuwa ni njia ya tembo (maeneo ya mapito ya wanyamapori) ambayo
 ilipitika kwa miaka mingi iliyopita na kwamba tembo wana kumbukumbu 
hata kama walipita njia hiyo kwa zaidi ya miaka 50 iliyopita. 
Imeelezwa
 kuwa njia hiyo ya mapito ya wanyamapori itakua ilitumiwa na wanyamapori
 kuhama eneo moja hadi jengine ikiwemo maeneo ya hifadhi ya Taifa ya 
Mikumi, Ruaha, Serengeti, Pori Tengefu la Rugwa na maeneo mengine ya 
hifadhi na kwamba maeneo hayo mengi kwa miaka ya hivi karibuni 
yameshaingiliwa na shughuli za kibinadamu ambazo hazisababishi tembo hao
 kusahau njia hizo au kutokuzitumia tena.
Tembo
 hao wakiwa ndani ya eneo chuo kikuu hicho cha Dodoma jana. Hakuna 
madhara yeyote yaliyoripotiwa kusababishwa na tembo hao na taratibu za 
kuwarudisha kwenye maeneo yao ya hifadhi zimeshaanza kuchukuliwa na 
uongozi wa Wizara ya Maliasili na Utalii ambapo Askari wa Wanyamapori 
wameanza zoezi la kuwafukuza kuwarudisha kwenye maeneo yao ya hifadhi.
Prof.
 Julius Nyahongo wa Chuo Kikuu cha Dodoma akitoa somo kwa wanafunzi wa 
chuo kikuu cha Dodoma namna ya kuchukua tahadhari juu ya ugeni wa tembo 
hao chuoni hapo.
Aliwaeleza wanafunzi hao kuwa mazingira ya chuoni hapo yataendelea kuwa salama kwakuwa tembo hao wapo katika njia yao ya mapito na pengine kumewahi kukucha kabla ya wao kufika mwisho wa safari yao, hivyo kwa msaada wa askari wa wanyamapori ambao wamewasili chuoni hapo itasaidia kuwaondoa tembo hao waweze kuendelea na safari yao hadi kwenye maeneo ya hifadhi.
Aliwaeleza wanafunzi hao kuwa mazingira ya chuoni hapo yataendelea kuwa salama kwakuwa tembo hao wapo katika njia yao ya mapito na pengine kumewahi kukucha kabla ya wao kufika mwisho wa safari yao, hivyo kwa msaada wa askari wa wanyamapori ambao wamewasili chuoni hapo itasaidia kuwaondoa tembo hao waweze kuendelea na safari yao hadi kwenye maeneo ya hifadhi.
Wanafunzi mbalimbali wa Chuo Kikuu cha Dodoma walikusanyika wakiwa na shauku ya kuwaona tembo hao.
Msafara
 wa viongozi mbali mbali wa Serikali ukiambatana na Askari Polisi na 
Askari wa Wanyamapori ukisogelea eneo walilokuwepo tembo hao kwa ajili 
ya kuanza kuwafukuza kutoka katika maeneo hayo ya chuo kwenda kwenye 
maeneo yao ya hifadhi.
Prof.
 Julius Nyahongo wa Chuo Kikuu cha Dodoma (wa pili kulia), Meneja 
Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania, Paschal Shelutete 
(wa tatu kulia) na maafisa wengine wa Serikali na vyombo vya ulinzi na 
usalama wakiangalia eneo walilokuwa wamejificha tembo hao chuoni hapo.
Askari
 wa wanyamapori wakiingia ndani ya eneo walilokuwa wamejificha tembo hao
 kwa ajili ya kuanza kuwafukuza eneo hilo kuelekea kwenye maeneo yao ya 
hifadhi. Imeelezwa kuwa pindi tembo hao watakapofukuzwa kwa milio maalum
 ya risasi hutafuta njia wanazozijua wenyewe za kurudi kwenye maeneo yao
 ya hifadhi.
Tembo
 hao wakianza kuondoka katika eneo hilo baada ya askari wa wanyamapori 
kuanza kuwaondoa eneo hilo kwa kutumia milio maalum ya risasi. (PICHA NA
 HAMZA TEMBA-WIZARA YA MALIASILI NA UTALII)

No comments