Binti wa miaka 15 abakwa na vijana wanne Jijini Mwanza.
Binti wa miaka 15 abakwa na vijana wanne Jijini Mwanza. 
 
 
 
 
 
 
Watu
 watatu wanashikiliwa na jeshi la polisi huku mwingine mmoja akiendelea 
kutafutwa kwa tuhuma za kumbaka binti mmoja mwenye umri wa miaka 15 
wilayani Ilemela, mkoani Mwanza.
Akitoa
 taarifa hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amesema 
kwamba tukio hilo limetokea tarehe 21/05/2017 majira ya saa moja kamili 
jioni katika maeneo ya mamlaka ya pamba, kata ya Kirumba ambapo inadaiwa
 kuwa binti huyo ambaye pia ni mkazi wa Kirumba alikuwa na mahusiano ya 
kimapenzi na mtuhumiwa aliyejulikana kwa jina moja la Phili na walipanga
 wakutane katika maeneo hayo.
Inasemekana
 kuwa binti huyo alikutana na mpenzi wake mahali hapo kisha walikwenda 
sehemu yenye jumba bovu kuzungumza, wakiwa kwenye eneo hilo ghafla 
walitokea vijana wengine watatu wakishirikiana na Phili na kuanza 
kumfanyia ukatili kwa kumbaka.
Inasemekana
 kuwa wakati wakiendelea na ukatili huo binti alipiga yowe akiomba 
msaada kutoka kwa wananchi, wananchi walifika eneo la tukio na kumuokoa 
binti na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa mmoja aitwaye Fredy Remigius 
kisha walitoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo.
Askari
 walifika katika eneo la tukio na kufanya msako mkali wa kuwatafuta 
watuhumiwa wengine huku wakishirikiana na wananchi na kufanikiwa 
kuwakamata watuhumiwa wengine wawili huku mmoja aliyekuwa na mahusiano 
ya kimapenzi na binti akifanikiwa kutoroka.
Amewataja
 watuhumiwa hao kuwa ni Fredy Remigius miaka 20, mkazi wa Kitangiri, 
Jackson Joseph miaka 17, mkazi wa Mlimani B na Frank Haruni miaka 18.
Kamanda
 Msangi amesema mahojiano na watuhumiwa waliokamatwa yanaendelea na 
pindi uchunguzi ukikamilika watafikishwa mahakamani na kwamba majeruhi 
aliyebakwa amepelekwa hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekou Toure kwa ajili 
ya matibabu na hali yake inaendelea vizuri.
No comments